Psalms 51:1-9

Kuomba Msamaha

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba.

1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.
2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.

3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 dDhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 eHakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 fHakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.

7 gNioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,
unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 hUnipe kusikia furaha na shangwe,
mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 iUfiche uso wako usizitazame dhambi zangu,
na uufute uovu wangu wote.
Copyright information for SwhNEN